Uzinduzi wa Album ya "Nimezaliwa Peke Yangu" ya Hussein Yamodel, 6.12.2014

Hussein Yamodel au UTAMU Yamodel kama wengine wanavyopenda kumuita anategemea kuzindua album yake itakayokwenda kwa jina la "NIMEZALIWA PEKE YANGU" ni moja kati ya nyimbo ambayo inatamba redioni.

Uzinduzi huo utakuwa chini ya kampuni ya T-MARC na utasindikizwa na bendi 2 kutoka Dodoma, Saki Star Band na TNC Band na hiyo itakuwa pande za Royal Village, Dodoma,siku ya Jumamosi ya tarehe 6.12.2014.

Pia ashaachia ngoma yake nyingine inayokwenda kwa jina la "Maisha ni Bahati" nayo ikiwa ni moja ya wimbo katika album hiyo.


KIINGILIO
VIP            -   10,000
KAWAIDA -     5000

Hebu sikiliza "Nimezaliwa Peke Yangu" ya Hussein Yamodel hapa

0 comments: